Kufuatia msiba wa mmoja wa waanzilishi wa bendi ya Osibisam Mac Tontoh [69], wenzetu
wa TBC walifanya kazi nzuri ya kuichambua historia ya kundi hilo lililoitambulisha
Afrika kwa dunia kunamo miaka ya 70 hadi kunyauka kwake mwanzoni mwa 90.
Katika maombelezo hayo TBC pamoja na mengine ilitoa changamoto la muziki unaotumia
ala halisi za muziki na umuhimu wa kuwa na chuo cha kufundisha vijana wetu upigaji
ala za muziki asilia na zile za Kizungu na nyinginezo tokea nchi mbalimbali duniani
ili kuwa na muziki tajiri badala ya muziki wenye mahadhi na mdundo wa kurekodiwa
unaofanya muziki wa Afrika kuwa kichekesho duniani tofauti na muziki wa Osibisa
uliokuwa tishio kwa miziki mingine duniani.
Ninaamini TBC na wadau wengine sasa watakwenda hatua moja na kuanzisha chuo cha ala
za muziki ili kunusuru kizazi hiki na muziki wa elektroniki usiyo na asili wala
No comments:
Post a Comment