Monday, September 19, 2011

Mass media needs new leaders and organizations

Mass Media needs various types of organizations and leaderships to enjoy economies of scale and prevent expenses that can be better utilized in growing bigger, profitable and more competent human capital.

Mass media needs new leaders and organizations

Mass Media needs various types of organizations and leaderships to enjoy economies of scale and prevent expenses that can be better utilized in growing bigger, profitable and more competent human capital.

Tuesday, April 19, 2011

Maudhui na sura ya gazeti hustahili kubadilika kila baada ya miaka miwili

Hivi unaweza kuwa na gazeti ambalo halibadili maudhui wala sura yake kwa miaka 2-3 na bado ukaamini unaweza ukashindana kwenye soko kwa kuuza jina la zamani tu?

Jiulize, tuwasiliane, tuongee na tufanye kazi! Bado kuna soko zuri tu mtu ukijiweka sawa kuanzia sasa maana msisimko wa demokrasia na katiba utazidi kuongezeka siku hadi siku!

Taarifa za Habari za dakika 10 zimepitwa na wakati

Mtanisahihisha kama ninakosea. Lakini ninaamini taarifa za habari za dakika 10 katika redio ni jambo lililopitwa na wakati.

Yapo maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi yenye masuala mbalimbali yanayoweza kuwa chachu ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiteknolojia na kiutamaduni endapo yanazungumziwa kwa kina na kwa upana wake na Watanzania wakajifunza kitu hapo na hivyo taarifa ya habari yenye uchambuzi wa dakika 20 au zaidi nadhani ndiyo iwe staili ya taarifa zetu za habari kuanzia sasa.

Ni bora uwe na taarifa mbili au tatu tu za habari kwa siku kuliko kuwa na taarifa 6 au zaidi ambazo hazina lolote jipya na ni za dakika chini ya 10 kila moja!

Redio za dini na siasa

HAKUNA hatari kubwa kama ile ya chombo cha habari cha kidini kuchanganya siasa na dini. Kumbukeni kina Radio Quran, Radio Kheri na Radio Imani yale ya Redio za kule Rwanda jamani!

Kama mpenzi wa redio hizo za dini hapo awali nilicacha kuzisikiliza kabisa zilipoanza kuhubiri siasa na tena zikionesha kuegemea waziwazi upande mmoja. Sikuhizi ninazisikiliza tu pale ninaposikia Kurani Tukufu inasomwa. Basi!

Wale wanaohusika na usimamizi wa vyombo vya habari watupie macho vyombo hivi kwa sababu kwa kweli kitaalamu na kimaadili vinahitaji msaada mkubwa tena wa haraka!

Mmm, Watangazaji kama hawa !

Unapomsikia mtangazaji wa redio au televisheni anayeshindwa kutofautisha kati ya 'ri' na 'li' katika kiswahili na wala sio Kiingereza, je, unakichukulia vipi chombo cha habari husika?

Saturday, January 8, 2011

REDIO YA MJI KASORO BAHARI NA AJENDA YAKE BINAFSI YA KATIBA

KUNA redio moja ya kidini inayotangaza kutoka Morogoro ambayo isipojiangalia itakuta inajiabisha siku hadi siku.

Jumamosi tarehe 7, Januari 2011 Redio hiyo ilikuwa na mahojiano na mwanasheria ambaye pamoja na kuwa hajui uandishi na uhariri wa habari unavyofanywa anakosowa waandishi wa habari.

Kubwa zaidi, hata hivyo, mwanasheria huyo tofauti na vigogo wa sheria nchini eti yeye kamuelewe rais kutaka kufanya marekebisho ya katiba na sio kuundwa kwa katiba mpya. Mmh.....kuna lao jambo.

Ni redio hiyo hiyo iliyomripoti Ndugu Issa Shivji kinyume kwa kusema eti amekataa kutungwa kwa katiba mpya. Jamani, endapo hamlitaki jambo kwa sababu zenu wenyewe msiwawekee watu maneno mdomoni. Sidhani kama Uislamu unakubali hilo. Unafiki na hasa redioni hauchelewi kuumbulika.

Tafuteni wahariri wa kiislamu (ambao wapo) wawanoeni ili mjenge Credibity kwanza kabla ya mambo mengine la sivyo watawasikiliza wengi leo, lakini kesho mtajikuta mnatangazia upepo nchi nzima!